Thursday 17 March 2016

JWTZ Wakana Kutuma Kikosi Uchaguzi Wa Marudio Z’bar

JWTZ Wakana Kutuma Kikosi Uchaguzi Wa Marudio Z’bar

Tarehe March 17, 2016
Baadhi ya wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania.
Baadhi ya wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania.
Jeshi la Wananchi wa Tanzania limekanusha vikali taarifa zilizoenea katika mitandao ya kijamii kuwa limepeleka wananjeshi wengi Visiwani Zanzibar kwa lengo la kudhibiti usalama kwenye uchaguzi wa marudio utakaifanyika machi 20,2016.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya mawasiliano Makao makuu ya Jeshi hilo  Upanga jijini Dar es salaam imebainisha kuwa  habari  hizo sio za kweli na zina lengo la kupotosha umma.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa JWTZ linao wanajeshi Visiwani Zanzibar ambao wakati wote kwa majukumu yake ya msingi ni pamoja na  Ulinzi  wa nchi.
Jeshi hilo limesisitiza kuwa  hakuna mwanajeshi  yeyote aliyeongezwa zaidi ya wale  waliopo visiwani humo.

clouds stream