Thursday 31 March 2016

Ubingwa Bado Kitendawili Msimbazi


Ubingwa Bado Kitendawili Msimbazi


Tarehe March 30, 2016
Kocha wa Simba Jackosn Mayanja
Kocha wa Simba Jackosn MayanjaKocha wa Simba Jackosn Mayanja
Jackson Mayanja anayekinoa kikosi cha Simba ambacho kipo kileleni katika msimamo wa ligi kuu ya Tanzania Bara amekuwa akisita kuzungumzia suala la ubingwa.
Mayanja ambaye ana kibarua kizito cha kuhakikisha Simba inarudisha heshima baada ya kukosa ubingwa kwa miaka minne amekuwa akishindwa kujibu swali hilo kama Simba inaweza kubeba kikombe hicho.
Kocha huyo kila alipoulizwa suala hilo amekuwa akijibu kuwa ni mapema sana kuzungumzia suala la ubingwa ambao kila timu unautolea macho.
“Kuongelea suala la ubingwa sahivi unajidanganya maana kuna timu zina pointi ambazo zinaweza kuchukua ubingwa pia,”amesema Mayanja


clouds stream