Friday 4 March 2016

Maalim Seif Atua Z’bar, Adai Polisi Sasa Ni Tawi La CCM

Maalim Seif Atua Z’bar, Adai Polisi Sasa Ni Tawi La CCM

Tarehe March 5, 2016
Maalim Seif akirejea Visiwani Zanzibar.
Maalim Seif akirejea Visiwani Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad aliyewasili  jana Zanzibar kutoka nchini India  kwa matibabu  amelishushia lawama Jeshi la Polisi visiwani humo kuwa limegeuka tawi la CCM.
Akizungumza na wafuasi wake waliofika kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume na baadaye kumsindikiza hadi nyumbani kwake Mbweni mjini hapa Maalim amedai kusikitishwa na kuona hujuma, watu wakipigwa na kujeruhiwa na Mazombi kila kukicha wakati Polisi wapo wanayaona na hakuna aliyeitwa kuhojiwa.
Aiidha, Maalim Seif alimlaumu, Dk Ali Mohamed Shein kuwa si muungwana akidai kuwa amekataa kuondoka madarakani.
Alisema la kushangaza zaidi ni kuona aking’ang’ania uchaguzi wa marudio, ilihali hakuna mantiki wala kifungu chochote cha sheria kinachohalalisha hatua hiyo.
Baadhi ya viongozi wa CUF waliohudhuria mapokezi hayo ni pamoja na Mansour Yussuf Himid, Nassor Ahmed Mazrui, Fatma Abdulhabibi Ferej na aliyekuwa mgombea mwenza wa Chadema chini ya mwavuliwa wa Ukawa katika urais wa Muungano, Juma Duni Haji.
Maalim Seif pia  alimtahadharisha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha asijaribu kulazimisha chama hicho kushiriki uchaguzi ‘batili’ wa marudio.
Uchaguzi wa marudio visiwani humo umepangwa kufanyika machi 20 mwezi huu,huku serikali ya Zanzibar ikisema maandalizi ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri.

clouds stream