Saturday 23 July 2016

Askari Barabarani Auawa Kwa Kupigwa Risasi Akiongoza Magari



Tarehe July 23, 2016
trafik1
Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajenti Mensah wa Kituo cha Polisi Oysterbay ameuawa usiku wa kuamkia leo  kwa kupigwa risasi akiwa kazini eneo la Sayansi Kijitonyama Jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Christopher Fuime amesema tukio hilo lilitokea majira ya saa mbili usiku na chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika.
Amesema kwa sasa wanafanya kazi kujua chanzo cha mauaji hayo ni nini na wahusika ni watu gani ili upelelezi wao uweze kuanza maramoja.

clouds stream