Sunday 31 July 2016

Wazungu Wamfata Mtanzania Aliyetengeneza Chopa

CmvplPZXYAA-E5n
Wakati Serikali ikipiga ‘biti’ kali sana kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) kwa yeyote yule anayejidai kutengeneza helikopta, Raia wa kigeni (Wazungu) kutoka nchini Afrika ya Kusini wamemtembelea Mkazi wa Tunduma, Mkoani Songwe, Adam Kinyekile, 34, ambaye ametengeneza helikopta na kumpatia mwaliko maalum wa kwenda kutembelea kiwanda chao cha kutengeneza chopa hizo huko bondeni.
Hivi karibuni, Kinyekile ambaye pia ni fundi magari alitumia ubunifu wake na kuunda helikopta ambayo ilivutia wengi sana na kupelekea Kiongozi wa Mwenge, George Mbijima akiwa Tunduma kumtembelea na kuweka jiwe la msingi katika eneo ilipo helikopta hiyo.
Ni dhahiri kuwa onyo la Serikali kupitia TCAA la kupiga marufuku mtu yeyote kujihusisha na utengenezwaji wa chopa bila kufuata utaratibu lilimhusu Bwana Adam na pengine kumkatisha tama asiendelee na utengenezaji wa chopa hiyo na sasa wazungu wamekuja kumvuta na si ajabu chochote atakachokivumbua zaidi tutaambiwa kuwa ni wazungu ndio wavumbua na si mtanzania ten

clouds stream