Friday 29 July 2016

Mwigulu Atema Cheche Kwa Mchina Aliyemtesa Mtanzania


Tarehe July 29, 2016Raia wa China akitemsa mtanzania.
Raia wa China akitemsa mtanzania.
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba ametua mkoa wa Geita kufuatia taarifa za mateso na mauaji yaliyodaiwa kufanywa na raia wa China wanaomiliki sehemu ya mgodi wa Nyamhuna uliopo Katoro, Geit
Aidha kwa muda wa wiki moja sasa imeripotiwa kutokea hali ya sintofahamu katika mgodi huo ambapo Mfanyakazi mmoja Raia wa Tanzania ametajwa kuteswa na kufanyiwa vitendo ya kinyama na mwajili wake ambaye ni raia wa china.
Katika Ziara hiyo Mwigulu Nchemba amejiridhisha kuwa kulikuwepo na tukio hilo la Mtanzania kuteswa na mwajiri wake, kipigo kilichosababisha kupoteza fahamu na siyo kifo.
Kufuatia Mtanzania kuteswa Nchemba alikwenda gereza la Geita mjini alikohifadhiwa kijana huyo kwa madai ya kushitakiwa na mwajiri wake kwa kosa la wizi lililosababishwa apigwe.
Katika mahojiano ya Waziri Mwigulu Nchemba na kijana huyo, Mwigulu alibaini kuwa kijana huyo aliyepo gerezani ndiye mhusika hasa wa tukio lile kwa uthibitisho wa makovu yaliyopo mwili mwake na mavazi aliyovalia wakati anateswa na akiwapo gerezani.
Waziri huyo alimchukua kijana aliyeteswa na kwenda naye mgodini kuwasaka waliopiga na kumpa mateso makali,ambapo aliwabaini Watanzania 5 ambao ni walinzi wa eneo hilo na Mchina mmoja walioshirikiana kumpiga.
Katika hatua nyingine Nchemba ameagiza wahusika wakamatwe mara moja na akaondoka nao kwa hatua zaidi za kisheria.Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba akiwa na kijana anayedaiwa kumtesa mtanzania.Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba akiwa na kijana anayedaiwa kumtesa mtanzaniaBaadhi ya wachina ambao ni Wahamiaji Haramu.Baadhi ya wachina ambao ni Wahamiaji Haramu.

clouds stream