Friday 22 July 2016

Vyuo Vikuu 6 Vyapigwa ‘Pini’ Kudahili Wanafunzi 2016/17


Tarehe July 22, 2016udom-660x330
Serikali imevizuia kwa muda jumla ya Vyuo Vikuu sita nchini kutofanya udahili wowote kwa mwaka wa masomo 2016/2017.
Vyuo hivyo ni pamoja na Interntaional Medical and Technological University (IMTU) ambacho haviruhusiwi kudahili wanafunzi katika kozi zote, St. Francis University College of Health and Allied Sciences (SFUCHAS) kozi zote, University of Bagamoyo (UoB) kozi zote, St. Joseph University College of Engineering (SJUCET) kozi zote.
Vingine ni University of Dodoma (UDOM) ambacho hakitaruhusiwa kudahili wanafunzi wa kozi ya udaktari, na State University of Zanzibar (SUZA) ambacho hakitaruhusiwa kudahili wanafunzi wa kozi ya udaktari.

clouds stream