Monday 4 July 2016

Maghembe Ashutumu Mawakala Utalii Kuendesha Mgomo Baridi Dhidi Ya VAT


Tarehe July 4, 2016tana4
Ikiwa ni siku chache tangu mawakala wa utali nchini kulalamika ongezeko la VAT katika sekta ya hiyo kumepelekea watalii kupungua, Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe ametoa onyo kwa mawakala wanaofungua akaunti nchi jirani ya Kenya kwa lengo la kukwepa kodi hiyo ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Waziri Maghembe amesema Kenya sio sehemu ya Tanzania na kwamba Tanzania sio koloni la Kenya hivyo hizi ni kodi za Tanzania hata kama Kenya imetoa tozo la kodi katika sekta hiyo na kusema kuwa Tanzania haiwezi kupangiwa kodi kwa Maendeleo ya taifa letu.
“Kinachoonekana hapa ni kama vile kuna propaganda na mgomo baridi kutoka kwa baadhi ya mawakala wanaotaka kuihadaa dunia ili iione Tanzania kutoza kodi hiyo ya VAT ni tatizo kubwa,” amesema.
Hatahivyo amedai kuwa Serikali inaendelea kuangalia mwenendo wa sekta hiyo ya utalii kwa muda wa mwezi mmoja au miwili ili kuona hali inakwendaje na baada ya hapo itafanya tathmini ya kina na kasha taarifa maalum itatolewa kwa Umma.
Mawakala hao walikaririwa hivi karibuni wakidai kuwa watalii wengi wamesitisha safari zao kuja nchini kufanya utalii na badala yake wameamua kwenda nchini Kenya ambapo kodi ya VAT imeondolewa.

clouds stream