Tuesday 26 July 2016

Safari Ya Yanga ‘CAF’ Yaota Mbawa


Tarehe July 27, 2016Donald Ngoma katika moja ya mechi na Medeama jijini Dar es salaam.
Donald Ngoma katika moja ya mechi na Medeama jijini Dar es salaam.
Klabu ya Dar es Salaam Young Africans imekubali kipigo cha goli 3­1 dhidi ya Medeama kutoka nchini Ghana.
Kipigo hicho cha Yanga dhidi ya Medeama kimezidi kufifisha safari ya Yanga kutinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ikiwa ni wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya Kombe la shirikisho barani Afrika.
Aidha, Magoli ya Medeama yamefugwa na Daniel Amoah dakika ya 7 na Abbas Mohammed aliyefunga magoli mawili dakika ya 22 na 37.
Kwa upande wa Yanga Simon Msuva ndiye aliyefunga goli la kufutia machozi kwa Yanga kupitia mkwaju wa penati dakika ya 24.
Kwa matokeo hayo Yanga wanaendelea kusalia na michezo miwili dhidi ya MO Bejaia ya Algeria watakaocheza nyumbani na TP Mazembe ya Kongo watakaocheza ugenini

clouds stream