Thursday 28 July 2016

Haya Ndiyo Majina Ya Wadaiwa Sugu Bodi Ya Mikopo


Tarehe July 28, 2016Wahitimu vyuo vikuu.
Wahitimu vyuo vikuu. Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB),imetangaza majina ya wadaiwa sugu ambao ambao mpaka hivi sasa hawajaanza kulipa mikopo waliochukua kipindi wanasoma.
Kwa mujibu wa Bodi hiyo wahitimu hao ambao majina yao yapo kwenye orodha wamevunja mkataba kutokana na sheria ya bodi hiyo No. 9 ya 2004 (kama ilivyorekebishwa) sehemu ya 19 (1). Aidha, wanataarifiwa kwamba, kulingana na sheria hiyo ya bodi (HESLB) No. 9 ya 2004, Bodi imedhamiria kutenda yafuatayo:­
(i) Bodi itachukua hatua za kisheria kulingana na kipengele cha 19 (a) (1) cha sheria ya bodi.
(ii) Mdaiwa atapewa penati ya 5% juu ya ile 5% iliyokua ikitozwa kabla kwa kila mwezi kwenye deni lililobakia au alilonalo.
(iii) Mdaiwa ataongezewa gharama za kumtafuta alipo ili alipe deni zilizoingiwa na bodi.
(iv) Mdaiwa atawekwa kwenye ‘blacklist’ na maelezo yake yatapelekwa kitengo cha kumbukumbu ya wakopaji na hivyo kushindwa kukopa sehemu nyingine yoyote.
(v) Mdaiwa atazuiliwa kupata udhamini wa Serikali au udahili wa masomo ya juu k
(vi) Maelezo yao yatapelekwa kwenye Wizara ya mambo ya ndani, kitengo cha Uhamiaji na balozi zote ambako watakataliwa safari zozote za kwenda nje ya nchi. 

clouds stream