Friday 22 July 2016

Samatta Atupia Kwa Penati Jana



Tarehe July 22, 2016Mbwana Samatta
Mbwana Samatta
Mbwana Samatta
Mshambuliaji  wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ‘Sama Goal’ amefunga penalti ya tatu timu yake, KRC Genk ya Ubelgiji  ikishinda kwa penalti 4-2 dhidi ya wenyeji Buducnost usiku huu Uwanja wa Pod Goricom mjini Podgorica, Montenegro katika mchezo wa marudiano Raundi ya Pili ya mchujo wa kufuzu hatua ya makundi ya Europ League.
Timu hizo zilifikia kwenye matuta baada ya sare ya jumla ya 2-2, Genk ikianza kushinda 2-0, mabao ya Neeskens Kebano kwa penalti dakika ya 16 na Samatta dakika ya 79 Alhamisi iliyopita na usiku huu Buducnost wamelipa kisasi kwa ushindi wa 2-0.

clouds stream