Tuesday 19 July 2016

Ibrahimovic Amtolea Uvivu Cantona


Tarehe July 19, 2016Zlatan Ibrahimovic.
Zlatan Ibrahimovic.
Zlatan Ibrahimovic.
Mshambuliaji mpya wa klabu ya Manchester United, Zlatan Ibrahimovic amejibu vijembe kutoka kwa gwiji wa Klabu hiyo Eric Cantona baada ya gwiji huyo kusema kuwa kuna mfalme mmoja tu katika klabu hiyo na siku zote atabaki kuwa yeye.
Siku chache baada ya Ibrahimovic kujiunga na klabu ya Man United akitokea Paris Saint German (PSG), Cantona aliandika katika mitandao ya kijamii ujumbe ufuatao:
“Just one last thing, there can only be one King in Manchester. You can be the Prince if you want to. And the No 7 is yours if you are interested. That is my welcome gift to you… The King is gone! Long live the Prince.”
Baada ya kauli hiyo, Ibrahimovic ameliambia gazeti la Aftonbladet, “I admire Cantona and I heard what he said.”
“But I won’t be King of Manchester. I will be God of Manchester,” ameongeza.
Wachezaji hao wote wawili wanajulikana kuwa na sifa ya utukutu huku Cantona aliondoka United akiwa hana maelewano mazuri na aliyekuwa kocha wake Ferguson na Ibrahimovic naye aliwahi kukwaruzana na Pep Guadiola wakati wapo Barcelona lakini pia aliwahi kufungiwa kwa kosa la kumpiga muamuzi.

clouds stream