Thursday 2 June 2016

DK SHEIN- SITOLEWI MADARAKANI KWA KUFANYA UGANGA WA KIENYEJI

RAIS wa Zanzibar ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Ali Mohamed Shein amewaambia wafuasi wa CCM kwamba wasihofu, kwani kamwe nchi haiwezi kuondolewa madarakani kwa kufanya uganga wa kienyeji.

Dk Shein alisema hayo wakati aliposalimiana na wafuasi wao katika Tawi la Wesha Shengejuu, ambalo ameahidi kulijenga upya baada ya kuchomwa na watu wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF).Ali-Mohamed-Shein1Alisema hayo baada ya wafuasi wa CCM, kudai kwamba viongozi wa CUF wamekuwa wakikesha kucha kutwa wakionekana kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kuiroga serikali ing’oke madarakani.

“Mkipata nafasi waambieni wapinzani kwamba nchi haiwezi kuondolewa madarakani kwa kufanya uganga wa kienyeji na kuroga…..,” alisema Dk Shein. Alisema uongozi wa nchi unapatikana kwa njia ya kushiriki katika uchaguzi unaoitishwa na Tume ya Uchaguzi kama ndiyo chombo halali kwa mujibu wa Katiba chenye majukumu ya aina hiyo.

Alisema kwamba CCM kiliamua kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa marudio, ulioitishwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutokana na kufutwa kwa uchaguzi wa Oktoba 25. “Hizo ndiyo njia sahihi ambazo zitamwezesha kiongozi wa nchi kushika dola baada ya kupata ridhaa kutoka kwa wapiga kura walioshiriki katika uchaguzi wa marudio,” alisema Dk Shein.

clouds stream