Thursday 30 June 2016

Kocha Omog Kusaini mkataba na simba Leo

Tarehe July 1, 2016
Joseph OmogJoseph Omog
Kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog anatarajiwa kufanya mazungumzo ya mwisho na uongozi wa Simba kabla ya kusaini Mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha klabu hiyo.
Omog na Simba SC wamefikia makubaliano baada ya mazungumzo ya awali kwa njia ya simu na barua pepe na Mcameroon huyo amekubali kuja kusaini Mkataba Dar es Salaam baada ya kutumiwa tiketi.
Simba itakuwa klabu ya pili kwa Omog kufundisha Tanzania baada ya awali kuwa na Azam FC, aliyoiongoza kwa msimu mmoja na nusu ikishinda mechi 30 kati ya 55 za mashindano yote, sare 14 na kufungwa 11.

clouds stream