Thursday 30 June 2016

Ukawa Watinga Bungeni Na Nguo Za ‘Msiba’, Mabango


Tarehe June 30, 2016Untitled
Untitled
Baadhi ya wabunge wanaotoka vyama vya siasa wakiwa nje ya ukumbi wa bunge baada ya kususia kikao cha bunge leo
Wabunge wa Kambi ya Upinzani leo wametoka nje ya ukumbi wa Bunge wakiwa na mabango mbalimbali yenye ujumbe wa kwenda kwa Rais Dkt John Magufuli na Naibu Spika Ackson Tulia.
Kabla ya kutoka nje, wabunge hao waliokuwa wamevalia mavazi yenye rangi nyeusi walisimama ndani ya ukumbi wa bunge kwa dakika chache huku wakiwa wamenyanyua mabango yao juu.
Huu ni muendelezo wa wabunge wa upinzani kususia vikao vinavyoendeshwa na naibu spika, Dkt Tulia wakidai kuwa amekuwa akikiuka kanuni za uendeshaji wa bunge.

clouds stream