Monday 20 June 2016

Yanga Wakubali kichapo kutoka kwa MO Bejaia



Tarehe June 20, 2016wachezaji wa Yanga wakimpongeza Donald Ngoma
Kutoka uwanja wa Unite Maghrebine mjini Bejaia pambano la kombe la shirikisho barani Afrika kundi A baina ya Wenyeji MO bejaia dhidi ya Yanga Afrika linamalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa goli 1 – 0, goli limefungwa dakika ya 20!Yanga wamemaliza mchezo huu wakiwa pungufu baada ya Haji Mwinyi kupewa kadi nyekundu.
Yanga wamecheza vizuri huku wakifanikiwa kutawala karibu kipindi chote cha pili lakini safu ya ushambuliaji hawakuweza kutumia nafasi hizo zakufunga.
 Yanga wameonekana kuwa bora zaidi usiku wa leo ukiachana na dosari za mwamuzi aliyekuwa akiwabeba wenyeji hawa wakija Dar watatakiwa kufungwa 3 – 0 iliYanga isonge mbele kwa uhuru.
Timu itarudi nchini Antalya Uturuki barani Ulaya hapo kesho kuendelea na kambi ambapo watarejea Tanzania tarehe 26 kuwasubiri TP Mazembe katika mchezo wa tarehe 28 June.

clouds stream