Monday 27 June 2016

Uingereza yatupwa nje michuano ya Ulaya

Timu ya taifa ya uingereza imetolewa katika michuano ya ulaya baada ya kufungwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Iceland. Mechi ya uingereza dhidi ya Iceland ilianza kwa kasi kubwa huku timu ya uingereza ikipata bao la mapema kwa njia ya mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa uingereza Raheem Sterling kuangushwa katika eneo la hatari na hivyo kuipatia timu yake Uingereza penati. Penati ya Uingereza ilipigwa na mchezaji Wayne Rooney ambaye hakufanya makosa na kuweka kambani mpira na hivyo Uingereza ikaongoza kwa bao moja katika dakika ya 4.




 Muda mchache baadae Iceland walifanya shambulizi na kufanikiwa kusawazisha kupitia mchezaji Ragnar Sigurdsson katika dakika ya 6.
Muda mchache baada ya Iceland kupata bao walifanya shambulizi linguine na kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 19 kupitia mchezaji Kolbeinn sigthorsson na hivyo kufanya matokeo kuwa uingerza moja na Iceland mbili.

Hadi kipindi cha kwanza kinaisha timu ya Iceland ilikuwa ikiongoza kwa mabao mawili dhidi ya bao moja la Uingereza.
Kipindi cha pili kilianza huku timu ya Uingereza ikifanaya mashambulizi mengi bila mafanikio. Kocha wa Uingereza Roy Hodgson alifanya mabadiliko ya wachezaji kwa kuwaingiza wachezaji Jack wilshere, Jamie vardy na kisha Marcus Rashford bila mafanikio. 
Hivyo hadi refa Damir Skomina anapiga kipenga cha mwisho timu ya Iceland ilikuwa ikiongoza kwa mabao mawili dhidi ya moja la Uingereza na hivyo kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali. 
Kufuatia kufanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali timu ya Iceland sasa itakutana na timu ya Ufaransa.



clouds stream