Monday 5 January 2015

BOKO HARAM WATEKA WAVULANA WENGINE 40

BOKO HARAM WATEKA WAVULANA WENGINE 40


Takriban wavulana 40 na vijana wadogo wameripotiwa kutekwa nyara na wapiganaji wa kundi la Boko haram Kazkazini mashariki mwa Nigeria.
Wakazi walio  kitoroka kijiji cha Malari na kuwasili katika mji wa Maiduguri siku ya ijumaa usiku wanasema kuwa kitendo hicho kilitekelezwa siku moja tu kabla ya mwaka mpya.
Watu waliojihami waliwasili katika kijiji hicho  wakiwa   katika gari aina ya pick up na kuwaagiza wanaume wote kutoka nje ili kuweza kusikiliza mahubiri ndipo waliwakamata na kuwateka vijana hao ambao walipelekwa  katika msitu jirani wa Sambisa.
Mwaka uliopita kundi hilo la Boko haram liliwateka nyara zaidi ya wasichana 200 kutoka shule moja ya bweni kazkazini mwa Nigeria.

clouds stream