Friday 16 January 2015

Gazeti la Charlie Hebdo lapigwa marufuku Senegal

Gazeti la Charlie Hebdo lapigwa marufuku Senegal


Gazeti la Charlie Hebdo lapigwa marufuku nchini Senegal.
Mwandishi wa  Habari  wa Gazeti la Charlie Hebdo lililopigwa marufuku nchini Senegal.
Senegal imepiga marufuku usambazaji wa jarida la Charlie Hebdo kote nchini humo. Nchi ya  Senegal ni nchi   ambayo  asilimia kubwa ni  waisilamu hivyo basi inadaiwa  kuwa uamuzi huo umepokewa kwa furaha na wananchi hao.
Nchi hio pia ina uhusiano wa karibu na Ufaransa ambayo ilikuwa mkoloni wake na majarida mengi ya kifaransa yanapatikana nchini humo.
Jarida Charlie Hebdo  limesambazwa kote duniani likuwa na kibonzo kinachomkejeli mtume akionekana kulia huku akishika bango linalosema ”Mimi ni Charlie” huku kichwa kinachofuata kikisomeka, ” Yote yamesamehewa”.

clouds stream