Thursday 19 February 2015

Mwili wa Mtoto Mwenye ualbino wapatikana msituni

Mwili wa Mtoto Mwenye ualbino wapatikana msituni


Mwili wa mtoto wa mwaka mmoja mwenye ulemavu wa ngozi Yohana Bahati aliyeporwa mikononi mwa mama yake juzi Mkoani Geita, umeonekana  jana jioni ukiwa umekatwa miguu na mikono yote na kufukiwa ardhini kwenye hifadhi ya msitu wa Biharamulo, Wilayani Chato.
Kwa mujibu wa  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Geita Joseph Konyo amesema mwili wa mtoto huyo umebainika jana majira ya saa 12:30 jioni ukiwa umefukiwa kwenye eneo ambalo linashamba la mahindi.
Mtoto mwingine mwenye ulemavu wa ngozi  aliyeporwa mwezi desemba mwaka jana  bado hajapatikana hadi leo licha ya jeshi la Polisi kungatangaza kutoa zawadi kwa atakayetoa taarifa zitakazo saidia kupatikana mtoto huyo.
Mauaji, ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi bado ni changamoto licha ya serikali kutafuta mbinu za aina mbalimbali kukabiliana  na tatizo hilo ikiwemo kuwapiga marufuku wapiga ramli.

clouds stream