Monday 9 February 2015

Yemen: Bomu lalipuka nje ya Ikulu, UN yatoa onyo

Yemen: Bomu lalipuka nje ya Ikulu, UN yatoa onyo

Ikulu ya Rais wa Yemen.
Ikulu ya Rais wa Yemen.
Bomu limelipuka nje ya ikulu ya rais wa Yemen, katika mji mkuu, Sanaa, mji ambao sasa unadhibitiwa na wapiganaji wa madhehubu ya Shia, wa Houthi
Inaarifiwa kuwa waasi wawili wa Houthi walijeruhiwa. Hapo jana wapiganaji hao walilivunja bunge kabla ya kudhibiti madaraka.
Sasa wapiganaji hao wamebuni halmashauri ya usalama kuongoza nchi hadi bunge la muda litakapoundwa.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema kuwa liko tayari kuchukua hatua zaidi, iwapo wapiganaji hao hawatarudi haraka kwenye mazungumzo, kuhusu kipindi cha mpito cha kuelekea kwenye demokrasi.
Baraza jipya limewataka wapiganaji wamuachilie huru rais wa Yemen, waziri mkuu, na baraza la mawaziri kutoka kifungo cha nyumbani.

clouds stream